Sat, 6 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwongozaji maarufu wa video nchini, Hanscana amewatolea uvivu wasanii kuhusu shows zao wanazofanya kwa kueleza kuwa wasanii wengi wana show mbaya na wanalilia shangwe baada ya kufanya show.
"Kuna tofauti kubwa sana kati ya show nzuri na shangwe, wengi mna show mbaya mnoo. Kila anayepanda analilia shangwe anasahau performance yaani atafanya vyovyote apate shangwe.
"Wengine wanavua hadi nguo apate ka clip watu wanampigia kelele apost IG ajifurahishe but not anything to improve performance," ameandika @hanscana_ kupitia Insta Story.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live