Sun, 7 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa Bongo Fleva Foby anasema aliwahi kwenda kwa Mganga baada ya mtu kumuambia jina lake limefukiwa chini na kurogwa kwa sababu muziki wake ni mkubwa lakini watu hawamjui.
Foby ameongeza kusema licha ya kwenda kwa Mganga lakini bado haamini katika upande huo akaamua kuachana navyo.
Foby ni miongoni mwa wasanii nyota wa bongo fleva wenye uwezo wa kuandika nyimbo za maudhui ya aina mbali mbali.
Foby pia huandikia mashairi wasanii wengine na ameshawaandikia watu kama Hamisa Mobeto "madam hero".
Foby ameshawahi ku-hit na nyombo kama Kitanda, bwana mkubwa na nyingine nyingi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live