Sat, 24 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa Muziki wa Bongofeva toka WCB Wasafi, Diamond Platnumz ametangaza kujiondoa katika tuzo za Bongo Music (Bongo Music Awards).
Diamond amejitoa kwa kuandika barua rasmi kwenda kwa waandaaji wa tuzo hizo Millenium Stars Entertainments.
Pia, Diamond alikuwa katika kipengele cha mtumbuizaji bora wa kiume (Best Male Perfomer) akichuana na Balaa Mc, Mr Blue, Joh Makini na Barnaba Classic.
Ikumbukwe sio mara ya kwanza kwa staa huyo kujitoa kwenye tuzo za hapa nchini alifanya hivyo katika tuzo za TMA zilizotolewa Aprili 2 2022 na kupewa tuzo ya heshima.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live