Kampuni maarufu ya mitindo na mavazi Dior imetangaza kusitisha kwa muda ushirikiano wake kibiashara na rapa Travis Scott kufuatia sakata la vifo vya mashabiki takribani 11 kwenye onesho lake la Astroworld Music Festival lililofanyika Novemba 5 mwaka huu.
Kampuni maarufu ya mitindo na mavazi Dior imetangaza kusitisha kwa muda ushirikiano wake kibiashara na rapa Travis Scott kufuatia sakata la vifo vya mashabiki takribani 11 kwenye onesho lake la Astroworld Music Festival lililofanyika Novemba 5 mwaka huu. Kwenye taarifa yao rasmi wamesema wamefikia uamuzi huo wa kusitisha ushirikiano wao na kampuni ya Travis Scott ‘Cactus Jack’ na kuahirisha uzinduzi wa bidhaa zao mpya ambazo zilikuwa ziingie sokoni msimu wa majira ya joto mwaka 2022.