Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Basata wazungumzia Dk Tulia kucheza wimbo uliofungiwa

29925 Basatapic TanzaniaWeb

Mon, 3 Dec 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Baada ya Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson kuonekana akicheza wimbo  Mwanza wa  msanii Rayvanny ambao umefungiwa, Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) limesema kitendo hicho hakimaanishi kuwa wimbo huo umefunguliwa.

Novemba 12, 2018 Basata ilitangaza kuufungia wimbo huo wa Rayvanny aliomshirikisha mwanamuziki Diamond Platnumz kwa maelezo kuwa unahamasisha masuala yasiyokubalika katika jamii.

Baraza hilo lilieleza kuwa linawasiliana na  mamlaka nyingine ili kuchukua hatua zaidi kwa kuwa tayari wimbo umeenea mitandaoni.

Siku chache baada ya kauli hiyo picha za video zimesambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii zikimuonyesha Dk Tulia akicheza wimbo huo sambamba na watu wengine wakifurahia ushindi walioupata kwenye michezo.

Huku wakiimba mashairi ya wimbo huo, wameonekana wakifurahi na kutabasamu huku kila mmoja akionyesha ujuzi wake wa kusakata muziki hali iliyowafanya wavutie kuwatazama.

Akizungumzia suala hilo katibu wa Basata,  Godfrey Mngereza amesema kitendo kilichofanywa na wabunge hao hakitengui uamuzi wa kufungiwa kwa wimbo huo kwa kuwa Basata wametekeleza wajibu wao kama wasimamizi wa sanaa.

“Kauli ya Basata haijabadilika kuhusu wimbo wa Mwanza kuwa haufai na umefungiwa. Kuhusu Wabunge sina cha kuongea kwani  hawa ni viongozi wetu na mimi ni mtumishi wa Serikali. Baraza tumetimiza wajibu wetu," amesema Mngereza.

 



Chanzo: mwananchi.co.tz