Wed, 17 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii wa kizazi kipya Elias Barnabas maarufu Barnaba, ametambulisha albamu yake mpya yenye nyimbo 18 katika tamasha alilolipa jina la Love Sounds Different.
Albamu hiyo ambayo muandaaji mkuu ni gwiji wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz, imezinduliwa ikiwa ni kumbukumbu ya miaka 18 tangu kuanza kazi ya muziki kwa mwanamuziki Barnaba.
Baadhi ya wanamuziki mashuhuri walioshirikishwa kwenye albamu hiyo ni Diamond Platnumz, Ali Kiba, Marioo, Rayvanny, Lunya, Lody Music Kusah, Dayoo, Khaligraph Joned, Mbosso, Lady Jaydee, Khadija Kopa na Platform.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live