Thu, 15 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanaume mmoja nchini Nigeria amevunja uchumba na kusitisha kufunga ndoa na mpenzi wake baada ya Bingi huyo kugoma kutaja jina la mtu aliyemnunulia iPhone 13 Pro Max.
Inasemekana wapenzi hao walikuwa kwenye hatua za mwisho za kufunga ndoa na Kijana huyo alivyomuona mpenzi wake na simu hio, aliuliza maswali yaliyokosa majibu na kuamua kufuta ndoa na uchumba.
Awali binti huyo alidai ni ndugu wa karibu ndiye aliyempa simu hio ila aligoma katu katu kutaja jina lake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live