Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Zaidi ya wafungwa 200 watoroka baada ya majambazi kuvamia gereza

Jela?fit=1200%2C749 Zaidi ya wafungwa 200 watoroka baada ya majambazi kuvamia gereza

Tue, 14 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wafungwa 240 wametoroka gerezani baada ya watu waliokuwa wamejihami na silaha kuvamia gereza moja katika eneo la Kabba-Bunu nchini Nigeria.

Wakati wa tukio hilo la Jumapili, Septemba 12 usiku, wavamizi hao walikabiliana na walinzi wa gerezaKisha walifanikiwa kuingia ndani ya gereza hilo baada ya kuwazidi nguvu maafisa hao.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Mamlaka ya huduma za magereza nchini Nigeria, ilisema kulikuwa na jumla ya wafungwa 294 katika gereza hilo wakati shambulio lilipotokea.

Wafungwa 240 kati yao walikuwa wakisubiri kesi zao, na 70 walikuwa tayari wamehukumiwa.

Taarifa kutoka nchini humo zinadai kuwa wakati wa tukio hilo la Jumapili, Septemba 12, wavamizi hao walikabiliana na walinzi wa gereza, na kisha walifanikiwa kuingia ndani ya gereza hilo baada ya kuwazidi nguvu maafisa hao.

Wakati huo kumekuwa na habari ambazo hazijathibitishwa kuwa kuwa maafisa wawili wa usalama waliuawa kwenye tukio hilo.



Hata hivyo, bado idara husika haijatoa taarifa kuhusu idadi ya watu waliouawa au majeruhi katika makabiliano hayo ya Jumapili usiku.

Tayari uchunguzi wa kuwasaka wafungwa waliotoroka umeanzishwa.

Zaidi ya wafungwa 1800 watoroka gerezani nchini NigeriaTukio hilo la Jumapili linakujia yapata miezi mitano baada ya lingine kutokea nchini humo mnamo Aprili 2021.

Maafisa wa polisi nchini Nigeria waliripoti kuwa zaidi ya wafungwa 1,800 wametoroka gerezani baada ya watu waliojihami kwa bunduki kuvamia gereza moja lililopo Mashariki mwa Owerri.

Kwa mujibu wa taarifa za BBC, washambuliaji hao walikuwa pia wamejihami kwa vilipuzi.

Msemaji wa polisi nchini humo aliambia vyombo vya habari kwamba, washambuliaji hao walitumia maroketi, maguruneti na silaha nyinginezo katika uvamizi huo, hakuna maafa yaliyoripotiwa.

Akitoa taarifa yake kwa umma, Rais Muhammadu Buhari alitaja shambulio hilo kuwa la kigaida na kutaka waliolitekeleza wakabiliwe vikali kisheria watakapokamatwa.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke