Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Zaidi ya polisi 1,000 kutumwa Naivasha kwenye mbio za Safari Rally

1b9b83a94011a2db Zaidi ya polisi 1,000 kutumwa Naivasha kwenye mbio za Safari Rally

Wed, 23 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Jeshi la nchi kavu litashirikiana na jeshi la hewa ili kuhimarisha usalama wakati wa mashindano hayo ya magari Idara hizo za usalama ni ikiwemo maafisa kutoka Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS), Idara Huduma za Wanyama Pori Kenya (KWS) na Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS)Zaidi ya madereva 50 wakiwemo Wakenya 34 watashikiri kwenye mashindano ya mwaka huu ya Safari Rally

Inspekta Jenerali wa Polisi Hillary Mutyambai ametangaza kuwa kikosi cha idara tofauti za usalama chenye zaidi ya maafisa 1,000 kitatumwa Naivasha.

Jeshi la nchi kavu litashirikiana na jeshi la hewa ili kuhimarisha usalama wakati wa mashindano hayo ya magari ambayo yameratibiwa kuanza Alhamisi, Juni 24, hadi Jumapili, Juni 27.

“Watahimarisha usalama kila wakati kwa wale washikadau wote wanaoshiriki. Mpango huo umegawanywa katika vitengo vitatu kabla ya hafla hiyo,” alisema Mutyambai.

Idara hizo za usalama ni ikiwemo maafisa kutoka Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS), Idara Huduma za Wanyama Pori Kenya (KWS) na Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS).

Mutyambai pia aliomba umma kushirikiana na maafisa wa usalama hususan wale wa trafiki kuhakikisha kuwa wasafiri wote wako salama.

Huku mamia wakitazamiwa kuhudhuria hafa hiyo, mashabikin wameombwa kufuata kanuni zilizowekwa na Wizara ya Afya kuzuia kuenea kwa COVID-19.

Takriban wageni 30,000 wanatazamiwa kukita kambi Naivasha huku hoteli zikiripotiwa kujaa.

Zaidi ya madereva 50 wakiwemo Wakenya 34 watashikiri kwenye mashindano ya mwaka huu ya Safari Rally.

Awali, Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i alitangaza kuwa barabara zinazoelekea mjini Nakuru zitafungwa wakati wa Mbio za Magari Duniani (WRC) Safari Rally zikikaribia.

Katika taarifa iliyochapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali Ijumaa, Juni 18, Matiang'i alisema barabara ya Kikope kuelekea Elementaita Village itafungwa kuanzia mwendo wa saa nane mchana hadi saa kumi na mbili jioni.

Waziri huyo pia aliagiza malori yote yenye zaidi ya uzani wa tani 3 kuzuiwa kutumia barabara tano kuu kati ya saa sita asubuhi na saa moja usiku.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke