Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yuko wapi jenerali? Rais Uhuru azuru mradi wa NMS bila Mohammed Badi

33508bec5676670b Yuko wapi jenerali? Rais Uhuru azuru mradi wa NMS bila Mohammed Badi

Fri, 2 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rais alizuru mradi wa kituo cha mabasi wa Green Park unaoendeshwa na shirika la mamlaka ya jiji

- Rais alikuwa ameandamana na kinara wa ODM Raila Odinga na maswali yakaibuka kuhusu alipo mkurugenzi wa NMS Mohammed Badi

- Badi ndiye kijana wa Rais katika kutekeleza matatizo ya jiji na huandamana naye kukagua miradi

Rais Uhuru Kenyatta Alhamisi Aprili 1 alizuru mradi unaoendeshwa na shirika la mamlaka ya jiji (NMS) wa Green Park Village.

Maswali yaliibuka alipo mkurugenzi wa NMS jenerali Mohammed Badi baada ya kukosa kuandamana na Rais kukagua mradi huo.

Rais alikuwa pamoja na kiongozi wa ODM Raila Odinga kwenye ziara hiyo ya Alhamisi ambapo alitangaza mipango kadhaa ya serikali katika juhudi za kutatua matatizo ya jiji.

Rais Uhuru Uhuru Kenyatta, Alhamisi alifanya ziara kukagua mradi wa kituo cha matatu cha Green Park chini ya mamlaka ya jiji NMS. Alikuwa ameandamana na kinara wa ODM Raila Odinga," NMS ilisema kwenye taarifa.



Badi hakuonekana popote katika picha zilizopakiwa kwenye mtandao wa NMS sawa na ukurasa wa Facebook wa Ikulu.

Jenerali amekuwa macho ya Uhuru katika masuala ya jiji tangu NMS iundwe na Rais amekuwa akiandamana naye kwenye miradi mingi.

Kukosekana kwake katika ziara ya jana kuliibua maswali kuhusu aliko na juhudi za TUKO.co.ke kupataa taarifa kutoka kwa NMS hazikuzaa matunda.

Upekuzi wa TUKO.co.ke ulionyesha Badi alikuwa kwenye umma Machi 18 wakati aliungana na Waziri wa Afya Mutahi Kagwe kuzuru kituo cha afya cha Lang'ata.

NMS iko chini ya serikali ya kitaifa kwa mujibu wa makubaliano yaliyowekwa na mkataba kati ya aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko na Ikulu.

Mradi wa Green Park ni baadhi ya miradi kadhaa ambayo Badi anatekeleza kama mojawapo wa ahadi kwa wakazi wa jiji kuhusu huduma bora.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke