Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Yafahamu majengo maarufu ya Freemason Kenya

Freemasonry  Jengo Yafahamu majengo maarufu ya Freemason Kenya

Wed, 12 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kuna baadhi majengo jijini Nairobi yanayokisiwa kujengwa na Freemason, huku majumba mengine yakitumika na wanasiasa, mengine yakiwa taasisi za elimu, kiuchumi au kidini.

Freemasonry ni shirika ambalo linaogopewa sana nchini humo, na wengi wanalihusisha na dhehebu linalomuabudu shetani.

Wakati Bosi wa Klabu ya Gor Mahia, Ambrose Rachier alipotangaza kwamba ni mwanachama wa Freemason, alipokea shutuma kali kutoka kila pembe nchini humo.

Baadhi ya washirika wa kibiashara wa Rachier, walianza kujitenga naye kwa kusema kwamba yeye ni mwanachama wa shirika hilo linaloogopewa na wengi.

Ila wengi hawajuia kwamba Freemasons walijenga baadhi ya majengo makuu jijini Nairobi.

Baadhi ya majumba hayo ya kihistoria ambayo yana nembo za Freemason ni pamoja na:

City Hall

Jengo hilo jeupe liko karibu na jengo la KICC. Kwa sasa jengo hilo ndilo makao makuu ya Gavana wa Kaunti ya Nairobi.

City Hall ilikamilishwa kujengwa na kufunguliwa kwa umaa miaka ya 1950. Hatimaye jengo hilo lilipanuliwa mwaka wa 1981 baada ya jengo la ghorofa 13 la City Hall Annex kujengwa kando yake.

Maktaba ya McMillan, ambayo iko kwenye makutano ya Wabera Street na Banda Street, ni maktaba ya umma.

Ndio maktaba kongwe zaidi jijini Nairobi na ni ya pili kwa ukongwe nchini Kenya baada ya maktaba ya Seif bin Salim iliyoko Mombasa.

Amyas Connell na Thornley Dyer ndio waliounda ramani ya majengo mapya ya Bunge yaliyotumika na utawala wa Uingereza kabla ya Kenya kujinyakulia uhuru.

Baada ya uhuru wa Kenya, majengo hayo yaligeuzwa jina na kuitwa 'New Parliament'.

Taasisi hiyo ilianzishwa ikiwa European Nairobi School. Hatimaye shule hiyo ilibadilishwa wakati Sir Edward Grigg alipokuwa gavana wa Kenya mwaka wa 1925 na kuitaka iwe shule ya wavulana wakubwa.

Grigg aliweka jiwe la msingi mwaka wa 1929 na kumpa mwanakandarasi Sir Herbert Baker, ambaye ni mwanachama wa Freemason, kuijenga.

Jiwe la msingi la the Church of All Saints liliwekwa mnamo Februari 1917.

Aliyejenga kanisa hilo Temple Moore alipendelea kuweka muundo wa Gothic kwenye ujenzi wake, na kukamilika mwaka wa 1952.

Hata hivyo, mwaka wa 1963, baada ya Kenya kujinyakulia uhuru ndipo Waafrika waliruhusiwa kutumia jumba hilo kuabudu.

Ukumbi wa Freemason

Wanachama wa kwanza wa freemason walikuja nchini humo kujenga kanisa la All Saints Cathedral.

Kwenye harakati hizo, walijenga Freemasons Lodge iliyoko Nyerere Road. Ilijengwa miaka ya 1930s na huonekana mahame.

Kenya National Archives ina rekodi za umma zaidi ya 4,0000. Jengo hilo kuu awali, lilikuwa ni benkil. Jengo hilo pia lina muundo wa kipekee na wa aina yake ikilinganishwa na majengo mengine.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live