Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wito wa maandamano kupinga vikwazo vya ECOWAS nchini Mali

ECOWAS MALIIIIIII Wito wa maandamano kupinga vikwazo vya ECOWAS nchini Mali

Wed, 12 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Serikali ya Mali imetoa wito wa kufanyika maandamano nchi nzima siku ya Ijumaa kupinga vikwazo vikali vilivyowekwa na jumuiya ECOWAS kutokana na kucheleweshwa kwa uchaguzi.

Taarifa ya Serikali ya mpito ya Mali iliotolewa baada ya kikao cha dharura cha baraza la mawaziri imesema vikwazo, ambavyo ni pamoja na kufungwa kwa mipaka na vikwazo vya biashara ,ni "vibaya" na kuwataka Wamali wote na hata wale wanmaoishi nje ya nchi kuandamana siku ya Ijumaa.

Viongozi kutoka Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ,ECOWAS, walikubali kuiwekea vikwazo Mali siku ya Jumapili, katika uamuzi ambao baadaye uliungwa mkono na mkoloni wa zamani Ufaransa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Serikali ya mpito huko Bamako ilisema itachukua hatua ya kukabiliana na vikwazo hivyo na kulinda uhuru na kuhifadhi mamlaka ya taifa la Mali.

''Hii haitusaidii kujiondoa kwenye mgogoro''

Mji wa Bamako ulibaki kuwatulivu leo jumanne na shughuli zinaendelea kama kawaida. Nouhoum Sangaré ,mkaazi wa Bamako amesema raia ndio watakaoumia na vikwazo hivyo.

''Kwa kuzingatia matatizo yote ambayo Mali imekuwa ikikabiliana nayo tangu mwaka 2012, adhabu hii ni kali sana. Ningetamani vikwazo viwe vyepesi zaidi. Vinginevyo vikwazo hivi ni vikali sana. Hii haitusaidii kujiondoa kwenye mgogoro.",alisema Sangaré.

Pamoja na kufunga mipaka na kuweka vikwazo vya kibiashara, pia walikata misaada ya kifedha kwa Mali na kuzuia mali ya nchi hiyo katika Benki Kuu ya Mataifa ya Afrika Magharibi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live