Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

William Ruto asema serikali ya 2022 itaundwa na mahasla

F52f17278cc5e2b4 William Ruto asema serikali ya 2022 itaundwa na mahasla

Thu, 22 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

DP Ruto alisema hatishiki na miungano ya siasa inayoundwa na wapinzani wake 2022 inapokaribiaAlisema kwa sasa Wakenya wanahitaji viongozi watakaoimarisha uchumi na kuboresha misha yaoRuto alikuwa akizungumza katika mji wa Machakos Jumatano wakati wa mkutano na wafanyabiashara wadogo kutoka kaunti hiyoSerikali ijayo itaundwa na mahasla ambao wako tayari kukabiliana uwanjani na muungano wowote wa upinzani, Naibu Rais William Ruto alisema.

Ruto alisema wapinzani wake wamegundua kuwa harakati za mahasla haziwezi kuzuilika, kwa hivyo wanazunguka wakitafuta kuunda muungano.

"Nilipowaambia kuwa serikali ya 2022 itaundwa na mahasla, walidhani ni utani. Sasa, wamejikuta katika pabaya na wanahangaika katika mikutano wakitafuta wale ambao wataungana nao," alisema.

DP alisema hatishiki na miungano hiyo na wala yanakoelekea mawimbi ya siasa katika siku za hivi karibuni.

Ruto alikuwa akizungumza katika mji wa Machakos Jumatano, Julai 21 wakati wa mkutano na wafanyabiashara wadogo kutoka kaunti hiyo.

Alisema lengo lake ni jinsi ya kuboresha maisha ya Wakenya wanaorauka kila kuchao kusaka lishe na kujenga uchumi wa taifa.



Read also

Raila Ataka Polisi Kuwajibika na Kuwakamata Wauwaji wa Wanawake, Wasichana

"Hatufadhaiki na mabadiliko ya kisiasa kati ya viongozi ambao lengo lao ni kujitengenezea nyadhifa. Lengo letu kama mahasla ni kuwawezesha Wakenya kiuchumi," alisema.

Ruto aliongeza aliwataka Wakenya kuwapuuza viongozi wa upinzani akisema kwamba hawana lolote ambalo wanawea kuwafaidi wananchi wa kawaida nalo.

Alisikitika kwamba utawala wa Jubilee ulikuwa na mipango kabambe kwa Wakenya wakati wa muhula wake wa pili lakini ulivurugwa na viongozi wa upinzani kupitia salamu za maridhiano.

"Kama chama cha Jubilee, tulikuwa na mipango mahsusi ya kuboresha maisha ya Wakenya kupitia utekelezaji wa ajenda Kubwa ya Nne. Lakini hilo lilivurugwa baada ya upinzani kujiunga nasi," alisema.

DP aliuliza upinzani kuomba msamaha kwa Wakenya kwa kuvuruga miradi ambayo ilikuwa na lengo la kuboresha maisha yao.

Waliokuwepo mkutanoni ni wabunge Victor Munyaka (Machakos Town), Vincent Musyoka (Mwala), Nimrod Mbai (Kitui Mashariki), na Rigathi Gachagua (Mathira).

Wabunge waliitaka jamii ya Wakamba kuchunga ili isipotoshwe na wanasiasa walaghai na badala yake kuunga mkono muungano utakaokuwa mamlakani 2022.

Read also

Hatubanduki Hadi Tuangamize Chama cha Jubilee, Didmus Barasa Asema

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke