Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

William Kabogo: Mt Kenya watakuwa na mgombea wa urais 2022

2f8f2122538af36b William Kabogo: Mt Kenya watakuwa na mgombea wa urais 2022

Mon, 10 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kabogo alisema eneo la Mt Kenya lina wingi wa kura na hivyo linafaa kujipanga kuwania urais ifikapo 2022

- Alipuuza mrengo wa Tangatanga akisema wanakutana na DP Ruto kujitetea na wala si kutetea maslahi ya Mt Kenya

- Kabogo alimtaka DP Ruto ajiondoe serikalini iwapo anahisi Rais Kenyatta ameanza kuenda segemnege

Aliyekuwa gavana wa Kiambu William Kabogo amesema eneo la Mlima Kenya 2022 watakuwa na mgombea wa urais.

Akiongea katika runinga ya Inooro Jumatatu Mei 10, Kabogo alisema eneo la Mt Kenya lina wingi wa kura na hivyo kuwa ya nguvu ya kisiasa.

Mwanasiasa huyo aliwataka wenzake katika Mt Kenya kujipanga wakisubiri 2022 kwani debe lao ndilo lenye uzito.

"Hata mimi nimetosha. Katiba inaruhusu kila mtu akiafikia matakwa ya kikatiba. Kura zetu ni mingi sana. Sisi tuko na asilimia kama 37 ya kura zote. Sisi ndio tutaamua ifikapo wakati huo. Kwa sababu sisi ndio wengi, tunafaa tuungwe mkono," alisema Kabogo.

Alipuuza mrengo wa Tangatanga ambao umekuwa ndani ya kambi ya Naibu Rais William Ruto akisema wanatetea maslahi yao.

"Hao wamekuwa hivyo. Hakuna kitu kipya wanafanya. Ni nani amewatuma hao waenda wakajadili maslahi ya Mt Kenya? Kabogo alisema.

Kabogo alitaka wanaTangatanga kupunguza siasa au wajitoe serikalini iwapo wanahisi Rais anaongoza visivyo.

"Rais na naibu wake waliomba kura pamoja. Manifesto yao ni moja, na kwa hivyo Ruto kama hakubaliani na manifesto ya Rais basi ajiondoe kwenye serikali," aliongeza Kabogo.

Alipigia debe mswada wa BBI akisema una manufaa makubwa kwa eneo la Mt Kenya haswa katika kutoa michuzi ya maendeleo.

"Hii niliisoma na kujua kuwa Mt Kenya tunaongezewa maeneo bunge na ndio nikaunga mkono mara moja. Saa hii unaona James Orengo ameanza kusema tutoa maeneo bunge. Na hiyo ikitolewa tutaiangusha mara moja," aliongeza

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemekem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke