Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wezi wa pikipiki wakamatwa na nyuki nchini Kenya

8f641fdfc6ea314b166887580268f28d Wezi wa pikipiki wakamatwa na nyuki nchini Kenya

Wed, 15 Sep 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

Katika hali isiyo ya kawaida, Mwanaume mmoja amekutana na balaa la kukamatwa na nyuki baada ya kuiba pikipiki katika eneo la Uasin Gishu nchini Kenya hata hivyo hakung'atwa na nyuki hao.

Baadhi ya mashuhuda na wakazi wa eneo hilo wamemsifu mmiliki wa piki piki hiyo James Wandera huku baadhi ya wakihusisha imani za kishirikina.

Taarifa zinaeleza kuwa baada ya Wandera kuibiwa pikipiki yake aliwasiliana na mganga wa kienyeji anayejiita Daktari Nyuki na ndipo alipowamwaga nyuki hao mpaka eneo husika la mwizi huyo, kisha kung’atwa na kuitupa pikipiki hiyo na hakuweza kukimbia mpaka wahusika walipofika na kumpeleka polisi.

Mwanamume anajilikana kama Wambura ni mmoja ya waliowahi kuwatumia Daktari Nyuki katika kazi zake anasema “baada ya kufanya Interview niliwasiliana na Daktari Nyuki wiki iliyofuata kuwa nimepita na nimepata kazi na nimekuwa mmoja ya wabosi,”amesema Wambura aliyewahi kumtumia Dk Nyuki.

Chanzo: www.habarileo.co.tz