Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wezi Warejesha Mali Waliyoiba Baada ya Kuandamwa na Kundi la Nyuki

0fgjhs3e2aj0jj2ag Wezi Warejesha Mali Waliyoiba Baada ya Kuandamwa na Kundi la Nyuki

Tue, 30 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wezi hao wawili wanaripotiwa kuiba mali hiyo wiki moja iliyopita huku aliyeibiwa akitafuta huduma za mganga

- Johnson Wanjala na Alfred Wanjala, waliumwa na nyuki kwa kilomita kadhaa wakirejesha mali ya Anita Chesang

- Wezi hao walivunja nyumba ya Chesang na kuiba televisheni, mtungi wa gesi na radio

- Nusra wawili hao wakatiziwe maisha na umati uliokuwa na hamaki lakini waliokolewa na polisi

Kulishuhudiwa kioja katika mtaa wa Langas, Kaunti ya Uasin Gishu siku ya Jumapili, Machi 28, baada ya wezi wawili kuvamiwa na kundi la nyuki na kulazimika kurejesha mali waliyoiba.

Wezi hao wawili wanaripotiwa kuiba mali hiyo mnamo Jumanne, Machi 23, huku aliyeibiwa akitafuta huduma za mganga.

Kwa mujibu wa gazeti la Taifa Leo la Jumatatu, Machi 29, wezi hao waliotambiliwa kama Johnson Wanjala na Alfred Wanjala, waliumwa na nyuki kwa kilomita kadhaa wakirejesha mali ya Anita Chesang.

Wezi hao walivunja nyumba ya Chesang na kuiba televisheni, mtungi wa gesi na radio.

Nusra wawili hao wakatiziwe maisha na umati uliokuwa na hamaki lakini waliokolewa na polisi kutoka Kituo cha Polisi cha Langas.

Kulingana na Chesang, alijaribu kutafta msaada wa polisi lakini juhudi zake ziligonga mwamba ndipo amtafuta mganga.

Mganga huyo alimuamuru atume picha ya mali yake iliyoibwa pamoja na udongo nje ua mlango wake ambao wezi hao walikanyaga achape kazi akiwa mbali.

Wezi hao walikiri kwamba walifanya kitendo hicho ili kujikimu kimaisha kutokana na uchumi.

Wakazi walifurahishwa na tukio hilo wakidai kwamba litasaidia kupunguza visa vya wizi mtaani humo wakisema kwamba watatumia huduma za mganga huyo endapo watapoteza mali yao.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke