Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wewe endelea kupiga duru, Rais Kenyatta amwambia DP Ruto

4b90ff9c8120a764 Wewe endelea kupiga duru, Rais Kenyatta amwambia DP Ruto

Sat, 26 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

DP Ruto Ijumaa Juni 25 alikashifu Rais Uhuru kutokana na mpango wa Jubilee kuungana na NASARais alionekana kumjibu Jumamosi akitaja cheche zake kama duru ambazo hazitamzuia kufanya chochoteNdoa kati ya Uhuru na Ruto imepasuka kiasi cha watoto kujua baba na mama hawapatani kabisaRais Uhuru Kenyatta Jumamosi Juni 26 alionekana kumtupia naibu wake William Ruto vijembe kuhusu siasa zake.

Akiongea Mombasa wakati wa kuzinduliwa kwa mradi wa uvuvi wa bilioni kumi, Rais alisema atatumia miezi yake ya mwisho afisini kuinua maisha ya Wakenya.

"Mambo haya tutatekeleza, nyinyi wenyewe mmeweza kuona tukiongeza idadi ya wananchi ambao wanapata stima kwa nyumba zao. Mambo haya ni ya kuhakikisha kuwa tuko na usawa katika taifa letu la Kenya

"Kwa hivyo kwa wale wanataka kuendelea kupiga duru wapige, sisi tuko kazini mpaka dakika ya mwisho. Na haja yetu sisi ni kuhakikisha kuwa taifa la Kenya litakuwa nzuri zaidi kuliko tulivyopata.



Rais alisema hulka ya viongozi kurushiana cheche za maneno kila wakati haina faida kwa yeyote.

Hii mambo ya matusi kila wakati sijui mimi ni hii na mimi ni hii haitakusaidia, kazi na jasho ndio inakusaidia . . . hawa wanawaambia vitu vya bure, lakini wacha niwacha hayo kwa sababu sikuja kusema hayo," aliongeza Rais.

Matamshi ya Rais yalijiri siku moja tu baada ya DP Ruto kumkashifu baada ya ripoti kuwa chama cha Jubilee kiko kwenye mpango wa kuungana na NASA chini ya Raila Odinga.

"Nyinyi watu ya Nakuru, eti sasa sisi Jubilee tunapelekwa NASA, kweli niwaulize, nyinyi mko na masaa ya kuenda kupewa stori na bwana kitendawili? Inawezekana kweli?" alisema DP wakati wa ziara yake Nakuru Juni 25.

Ruto na Uhuru wamekuwa hawapatani tangu kinara wa ODM Raila Odinga aingie kwenye serikali kupitia mkataba wa handisheki.

Sasa ndoa yake na Rais ilipasuka kiasi kwamba wao hurushiana cheche za maneno pasi kuficha hata watoto wao kuhusu masaibu yao.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke