Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini DRC (CENI) Denis Kadima amesema kuwa wapiga kura wote waliosajiliwa rasmi wataruhusiwa kushiriki katika uchaguzi mkuu utakaofanyika wiki ijayo hata ikiwa kadi za kupigia kura zimeharabika
Kuali hiyo ya CENI imeungwa mkono na uamuzi wa Mahakama ya Katiba ambayo imeyakataa madai yote ya kuahirisha uchaguzi yaliyotolewa na wagombea Urais wa upinzani
Mahakama imesema kuwa madai yao hayana msingi na mchakato wa uchaguzi utaendelea kama ilivyopangwa
Kumękuwa na wasi wasi kuwa idadi kubwa ya wapiga kura huenda wasishiriki uchaguzi huo baada ya maelezo kwenye kadi zao kufutika hiyo kauli ya Tume inaweza kuleta matumaini kwa wapiga kura
Tume ya uchaguzi imekuwa ikiendesha shughuli ya kuwapa wapiga kura wałiosajiliwa kadi mpya ikiwa kadi żao zimeharibika łakini zoezi lenyewe limekuwa likienda pole pole kutokana na idadi kubwa ya watu waliojitokeza ili kupata kadi mpya
Kadima ameongeza kuwa hadi sasa hawajafanikiwa kupata ndege za kutosha kusafirisha vifaa vitakavyotumika wakati wa uchaguzii hadi maeneo yote
Siku mbili zilizopita CENI iliiandikia serikali ya DRC na Umoja wa Mataifa kuipa misaada ya ndege ili kufanikisha shughuli ya kusafirisha vifaa vya kupigia kura