Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Weah rais wa kwanza kushindwa uchaguzi Liberia

Weah Rais Wa Kwanza Kushindwa Uchaguzi Liberia Weah rais wa kwanza kushindwa uchaguzi Liberia

Sat, 18 Nov 2023 Chanzo: Bbc

Kiongozi anayeondoka madarakani nchini Liberia George Weah anaweka historia nchinni humo kwa kuwa rais wa kwanza kushindwa katika kinyang’anyiro cha kuwania muhula wa pili madarakani.

Weah ambaye alijizolea umaarufu mkubwa nchini mwake na duniani kwa ujumla wake kwa kucheza soka katika ngazi za juu zaidi kimataifa aliingia madarakani mwaka 2018 kwa muhula wa kwanza na alikuwa akitaraji kuendelea na awamu ya pili mwaka huu kabla ya kubwagwa na mpinzani wake Joseph Bokai katika uchaguzi wa marudio uliofanyika wiki iliyopita.

Bokai amepata ushindi mwembamba wa asilimia 50.89 ya kura dhidi ya asilimia 49.11 alizopata Weah. Ikiwa takriban kura zote zimeshahesabiwa, Bokai amemzidi Weah kwa takribani kura 28,000. Takwimu hizi zinaonesha ni kwa namna gani mchuano baina ya wawili hao ulivyokuwa mkali.

Kwa upande wa Bokai ushindi wake pia umeweka historia nchini humo kwa kuwa mtu wa pili kukirudisha chama tawala cha zamani madarakani. Na kwa Bokai binafsi ushindi wake ni kisasi dhidi ya Weah ambaye alimshinda katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2017.

Weah sasa anatarajiwa kuondoka madarakani mwezi Januari baada ya kuapishwa kwa rais mteule Bokai.

Chanzo: Bbc