Tue, 24 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Aliyekuwa Waziri wa Elimu nchini Kenya Prof. George Magoha amefariki dunia leo Januari 24, 2023 katika hospitali ya Nairobi akiwa na umri wa miaka 71 baada ya kuugua kwa muda.
Prof Magoha aliapishwa mnamo Machi 26, 2019 akiongoza wizara ya Elimu na kuhudumu hadi Oktoba 27, 2022 wakati Rais William Ruto alipomtaja mrithi wake.
Hivi majuzi tu alijiunga na Chuo Kikuu cha Maseno kama profesa katika Idara ya Shule ya Tiba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live