Mon, 19 Oct 2020
Chanzo: habarileo.co.tz
Waziri wa Afya wa Afrika Kusini ‘Sauzi’ Zweli Mkhize na Mkewe DkMay Mashego wamepata ugonjwa wa covid 19 unaosababishwa na virusi vya corona ambapo kwa mujibu wa taarifa kutoka Ofisi yake imethibitisha.
"Sasa niko katika karantini nyumbani, na mimi na mke wangu tunabaki na matumaini kwamba tutapona kabisa kutoka kwa virusi hivi," Mkhize alinukuliwa akisema katika taarifa hiyo.
Taarifa hiyo imetolewa mara baada ya Mkhize kupimwa siku ya Jumamosi baada ya kuonyesha dalili dhaifu.
Chanzo: habarileo.co.tz