Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waziri mkuu wa Niger anatarajia kufikia makubaliano na Ecowas

Waziri Mkuu Wa Niger Anatarajia Kufikia Makubaliano Na Ecowas Waziri mkuu wa Niger anatarajia kufikia makubaliano na Ecowas

Tue, 5 Sep 2023 Chanzo: Voa

Wazir Mkuu mpya wa Niger amesema kuna matumaini ya kufikia makubaliano baina ya uongozi wa jeshi mjini Niamey na Jumuiya ya Kiuchumi ya nchi za Magharib Ecowas.

Ali Mahamane Lamine Zeine, aliyeteuliwa kwa wadhfa huo na serikali ya kijeshi, alikuwa akizungumza kwa mara ya kwanza hadharani katika mkutano na wandishi habari katika mji mkuu Niamey.

“Hatujasitisha mazungumzo na Ecowas, bado tunaendelea kujadiliana. Tuna matumiani ya kufikia makubaliano katika siku zijazo,” aliwaambia wandishi habari.

Jumuiya ya Ecowas imetishia kutumia nguvu kurejesha utawala wa kiraia nchini humo baada ya jeshi la kumlinda rais kufanya mapinduzi mnamo Julai 26 na kumng'oa madarakani rais Mohamed Bazoum.

Kamanda wa mapinduzi hayo, jenerali Abdourahmane Tchiani, alijitangaza kama kiongozi mpya na kumweka kizuizini rais Bazoum na familia yake.

Lamine amesisitiza kuwa uongozi wa kijeshi utajihamai kutokana na uvamizi wowote.

Waziri Mkuu huyo pia aliongeza kwamba uongozi mpya bado unaendelea kufanya mazungumzo na Ufaransa ili kuondoa vikosi vya Ufaransa vilivyoko nchini humo. Ufarsana ina takriban wanajeshi 1,500 nchini Niger, baadhi yao wakiwa katika kambi moja karibu na mji mkuu.

Ufaransa imekataa kutambua viongozi waliofanya mapinduzi na kusisitiza kwamba bado inatambua tu uongozi wa rais Bazoum kama serikali halali, hatua ambayo imezua ghadhabu miongoni mwa uongozi wa kijeshi mjini Niamey.

Serikali hiyo imejibu kwa kutangaza kumfukuza balozi wa Ufaransa nchini humo huku mamia ya raia wanaounga mkono mapinduzi wakiandamana kutaka balozi huyo aondoke nchi hiyo.

Chanzo: Voa