Khartoum, Somalia. Waziri wa Mambo Ndani nchini Somalia, Mohamed Abdirahman na Gavana wa Jimbo la Puntland, Abdisalan Hassan Hersi wamejeruhiwa katika shambulio la kigaidi.
Viongozi hao pamoja na kamanda wa zamani wa polisi na raia mmoja nao pia walijeruhiwa kwenye mashambuo hilo.
Shambulio hilo la kujitoa muhanga lilitokea Jumapili iliyopita Machi 19, linadaiwa kutekelezwa na kundi la al-Shabab katika Mkoa wa Nugaal, Somalia
Watu waliokuwa karibu na neo hilo walisema walisema walishuhudia mwanaume mmoja akijirusha mbele ya gari walilokuwa viongozi hao na kulipuka.
Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi nchini Somalia, mtu huyo aliyekuwa amejivisha mabomu hakufahamika mara moja.
Taarifa hiyo ilisema watu wote waliokuwa katika gari hiyo walijeruhiwa vibaya na kupelekwa katika Hospitali ya Mkoa Nugaal kwa matibabu.
Pia Soma
- Wafanyakazi benki ya Akiba wahukumiwa kulipa faini, fidia ya Sh62 milioni
- Walioambukizwa corona Rwanda wafika 70
- Ilani ya uchaguzi yatumika kwa mara ya pili
Kwa miongo kadhaa kundi la al-Shabaab limekuwa likitekeleza mauaji nchini Somali ambako mwaka 2011 Jeshi la nchi hiyo lilitangaza kuondoa ngome yake katika mji mkuu wa Mogadishu.
Hata hivyo, kundi hilo bado linadhibiti maeneo makubwa nje ya Mogadishu na mara kwa mara limekuwa likifanya mauaji ya watu katika maeneo ya mikusanyiko, hoteli na usafiri wa umma.