Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waziri Mkuu wa Misri akataa wito wa wakimbizi wa Kipalestina kwenda Sinai

Waziri Mkuu Wa Misri Akataa Wito Wa Wakimbizi Wa Kipalestina Kwenda Sinai Waziri Mkuu wa Misri akataa wito wa wakimbizi wa Kipalestina kwenda Sinai

Tue, 31 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Waziri Mkuu wa Misri amekataa mpango wowote wa watu waliohamishwa kutoka Gaza kuhamishwa kwa wingi katika rasi ya Sinai nchini Misri.

Vyombo vya habari nchini Israel vimeripoti kuwa baadhi ya maafisa wa Israel wanataka kuwahamisha raia kutoka Gaza hadi kaskazini mashariki mwa Misri.

Lakini, katika ziara yake Kaskazini mwa Sinai, Mostafa Madbouly anasema hakuna mzozo wa kikanda unapaswa kutatuliwa kwa gharama ya Misri.

Kama ukumbusho, vivuko vya Israel kuingia Gaza vimefungwa, kivuko cha Rafah kinachodhibitiwa na Misri ndiyo njia pekee inayoweza kuwawezesha raia kuondoka Gaza.

Chanzo: Bbc