Tue, 31 Oct 2023
Chanzo: Bbc
Waziri Mkuu wa Misri amekataa mpango wowote wa watu waliohamishwa kutoka Gaza kuhamishwa kwa wingi katika rasi ya Sinai nchini Misri.
Vyombo vya habari nchini Israel vimeripoti kuwa baadhi ya maafisa wa Israel wanataka kuwahamisha raia kutoka Gaza hadi kaskazini mashariki mwa Misri.
Lakini, katika ziara yake Kaskazini mwa Sinai, Mostafa Madbouly anasema hakuna mzozo wa kikanda unapaswa kutatuliwa kwa gharama ya Misri.
Kama ukumbusho, vivuko vya Israel kuingia Gaza vimefungwa, kivuko cha Rafah kinachodhibitiwa na Misri ndiyo njia pekee inayoweza kuwawezesha raia kuondoka Gaza.
Chanzo: Bbc