Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waziri Matiang'i ammaliza DP Ruto kwa kuanika mali yake

D33067e2d690917a Waziri Matiang'i ammaliza DP Ruto kwa kuanika mali yake

Thu, 2 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Alhamisi Septemba mbili yamechapisha taarifa iliyotolewa katika bunge na Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i kuhusu usalama wa naibu rais William Ruto.

Matiang'i alikuwa bungeni kuelezea hatua ya kuwaondoa walinzi wa GSU kutoka makao ya DP Ruto Karen na Sugoi.

People Daily

Taarifa kuu kwenye gazeti hili ni kuhusu vile DP Ruto alijikaanga baada ya kutaka Waziri Fred Matiang'i na mkuu wa polisi Hillary Mutyambai kuelezea kuhusu kuondolewa kwa maafisa wa GSU Karen.

Wawili hao walifika bungeni Jumatano Septemba 1 na kuweka wazi idadi ya maafisa ambao wanalinda DP Ruto pamoja na mali yake.

Katika kuelezea hilo, Matiang'i aliweka wazi mali ambayo inamilikiwa na DP Ruto jambo ambalo limekera Ruto na kusema ni hatua nyingine ambayo inamuweka katika hatari.

Star

Gazeti la Star ni kuhusu Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji ambaye analalamikia vizingiti katika kupigana na ufisadi.

Alisema siasa zimekuwa zikitumiwa kuhujumu kazi yakena hivyo kufanya yeye kushindwa kutekeleza kazi yake vilivyo.



Kuna taarifa pia kuhusu Karen ambapo taarifa ya Waziri Fred Matiang'i bungeni imekera na msemaji wa DP Ruto alipuuzilia aliyoyasema waziri huyo.

Taifa Leo

Mhariri wa gazeti hili anasema itakuwa ngumu kwa DP Ruto kuendelea kuuza injili yake ya Hustler baada ya mali yake kuwekwa wazi.

Amempa jina la Hasla Bandia baada ya mali yake ya mabilioni kuanikwa na Waziri Fred Matiang'i.

Daily Nation

Duru zimearifu gazeti hili kuwa Waziri Matiang'i aliambia kamati ya bunge kuwa DP Ruto amekuwa akiwatumia maafisa wake wa ulinzi visivyo.

Alidai tayari DP amewapa wandani wake Oscar Sudi na Aisha Jumwa baadhi ya maafisa wake.

Alisema hilo lilifanyika baada ya walinzi wa wawili hao kuondolewa walipohusishwa na kesi za uhalifu.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke