Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wazazi wakataa kumlipia binti yao karo ya chuo kikuu wakidai elimu ni dhambi

0fgjhs5rp7iov5n2e Wazazi wakataa kumlipia binti yao karo ya chuo kikuu wakidai elimu ni dhambi

Wed, 7 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kariiri alisema wazazi wake walitishia kumkana na kutomshughulikia iwapo akijiunga na chuo kikuuMsimamo wa wazazi hao ni baada ya kujiunga na dini mpya ya Kabonokia mwaka 2019, ambayo inaamini kuwa elimu na ajira ni kinyume cha bibiliaKatika madhebehu ya Kabonokia, waumini hawaruhusiwi kuwa na vitambulisho vya kitaifa, kutafuta kazi, kupiga kura na kuhesabiwa

Wazazi kutoka eneo la Gatue, kaunti ya Tharaka Nithi, wamemshangaza binti yao wakitishia kumlaani endapo atajiunga na chuo kikuu.

Wazazi hao wa Doris Kariiri ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zetech, Nairobi, wamekatisha matumaini yake ya kukamilisha masomo.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, Kariiri alisema wazazi wake walitishia kumkana na kutomshughulikia iwapo akijiunga na chuo kikuu.

"Wazazi wangu wamekataa kunilipia karo, kodi ya nyumba na hata kunipa pesa za kujikumu nikiwa shuleni," alisema Kariiri.

Msimamo wa wazazi hao ni baada ya kujiunga na dini mpya ya Kabonokia mwaka 2019, ambayo inaamini kuwa elimu na ajira ni kinyume cha bibilia.

Hivyo, wazazi wa Kariiri waliamua kuwa watoto wao hawataendelea na masomo yao.

Serikali kuingilia katiChifu wa eneo hilo la Gatue, Nyaga Mwinja alisema atashirikiana na polisi pamoja na idara zingine husika kuwasaida watoto hao kukamilsha masomo yao.

Mwinja alionya kuwa wazazi hao watachukuliwa hatua za kisheria akiongezea kuwa madhebehu hayo ni tishio kwa elimu.

Dini ya Kabonokia

Katika madhebehu ya Kabonokia, waumini hawaruhusiwi kuwa na vitambulisho vya kitaifa, kutafuta kazi, kupiga kura na kuhesabiwa.

Dini hiyo pia ina matawi yake katika kaunti za Meru, Kitui na Embu.

Mwanzilishi wa dini hiyo, Gitonga M'Mpurunguru aliaga dunia Septemba 2020 akiwa na umri wa miaka 71.

Mratibu wa Maendeleo ya Wanawake katika kaunti ya Tharaka Nithi, Aniceta Kirega alisema mipango imeanzishwa kuvunja dini hiyo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke