Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wavuvi wapata jiwe la thamani ya mamilioni ya pesa ndani ya tumbo la nyangumi

E69101cec184660d Wavuvi wapata jiwe la thamani ya mamilioni ya pesa ndani ya tumbo la nyangumi

Sat, 5 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kitu hicho chenye harufu kinachojulikana pia kwa jina ambergris - kilitoka ndani ya mzoga wa mnyama huyo wa baharini katika Ghuba ya Aden

- Kwa mujibu wa The India Times, Paundi 280 za jiwe hilo lenye thamni ziliripotiwa kuuziwa mfanyabiashara katika Falme za Kiarabu kwa $ 1.5 milioni sawa na 161.8 milioni pesa za Kenya

- Huko Marekani ukusanyaji na uuzaji wa ambergris ni haramu kwa sababu ni bidhaa kutoka kwa spishi iliyo hatarini kwa sera zilizowekwa na Utawala wa Baharini na Angani

Maisha ya kundi la wavuvi nchini Yemeni yamebadilika kutokana na matapishi ya thamani yaliyotoka ndani ya nyangumi.

Pia Soma: Huyu Hapa Ndiye Mae C. Jemison, Mwanamke wa Kwanza Mweusi Kufika Anga za Mbali

Kitu hicho chenye harufu kinachojulikana pia kwa jina ambergris - kilitoka ndani ya mzoga wa mnyama huyo wa baharini katika Ghuba ya Aden, kulingana na BBC.

Ndani ya tumbo la nyangumi wa manii aliyeelea kulikuwa na paundi 280 za ambergris, ambayo ni dutu dhabiti ya kumengenya ambayo hutumiwa katika viwanda vya kutengeneza manukato kupunguza harufu, Britannica iliripoti.

Madini hayo huundwa wakati nyangumi wa manii anaposhindwa kumeng'enya midomo kutoka kwa samaki aina ya ngisi na dome, kulingana na nadharia za hivi karibuni ambazo zinaamini ambergris imerejeshwa kama mfumo wa kinga kufuatia kuwasha kwa matumbo.

Wanaume thelathini na watano walimvuta nyangumi aliyekufa wakitarajia alikuwa na ambergris kutokana na harufu yake, mmoja wa wavuvi alielezea katika mahojiano ya video na BBC.



Kwa mujibu wa The India Times, Paundi 280 za jiwe hilo lenye thamni ziliripotiwa kuuziwa mfanyabiashara katika Falme za Kiarabu kwa $ 1.5 milioni sawa na 161.8 milioni pesa za Kenya.

Huko Marekani ukusanyaji na uuzaji wa ambergris ni haramu kwa sababu ni bidhaa kutoka kwa spishi iliyo hatarini kwa sera zilizowekwa na Utawala wa Baharini na Angani.

Pesa zilizotokana na jiwe hilo zimetumiwa na wavuvi hao kununulia magari, nyumba na boti huku wakitoa misaada mbalimbali kwa ajili ya kijiji chao.

Umoja wa Mataifa unaripoti kuwa Yemen ina idadi ya watu karibu milioni 24.1 na 80% wanasemekana kuwa "wanahitaji misaada ya kibinadamu na ulinzi."



Pia Soma: China Inapojitahidi Kujenga Jumuiya ya Binadamu yenye Hatma ya Pamoja, Marekani Nayo Inatenda Kinyume

Kando na kundi hili la wavuvi wa Yemen, watu wengine kote Mashariki ya Kati na Asia ya Kusini wamefanikiwa kupata vipande vya ambergris ambavyo tamani yake ni mamilioni ya dola.

Mnamo mwaka wa 2016 Gulf News iliripoti kwamba wavuvi watatu huko Oman walipata na kuuza pauni 176 za ambergris, ambayo ilikuwa na thamani ya karibu dola milioni 3 sawa na KSh 324 milioni. Miaka minne baadaye, mvuvi wa Thai alipata na kuuza kitita chake cha pauni 220 ambacho kilikuwa na thamani ya karibu $ 3.3 milioni, kulingana na Daily Mail.

Leo, ambergris hutumiwa kama kihifadhi katika manukato na bidhaa zingine zenye harufu. Harufu ya aina hii inaripotiwa kutumika katika bidhaa nyingi za manukato za Uropa na Mashariki ya Kati, kulingana na Fragrantica - ensaiklopidia ya manukato mtandaoni.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Pata Matukio Motomoto Kupitia Video Hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke