Wed, 15 Sep 2021
Chanzo: millardAyo
Serikali Nchini Zimbabwe imewapiga marufuku wafanyakazi wa Utumishi wa Umma kwenda Maofisini ambao hawajachanja chanjo ya Covid-19. ikiwa ni njia ya kupunguza kasi ya maambukizi .
Waziri wa Habari, Monica Mutsvangwa amesema Baraza la Mawaziri la Nchi hiyo limekubaliana kuwa Wafanyakazi waliochanja pekee ndio wanaruhusiwa kuripoti makazini.
Hata hivyo, Katika siku zijazo wamepanga kuwa Watu waliochanja pekee ndio wataruhusiwa kuhudhuria kwenye nyumba za Ibada na kwenye Migahawa ya chakula.
Chanzo: millardAyo