Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu wengine 719 wapatikana na virusi vya COVID-19 huku 800 wakipona

B7f44183c6696faf.jpeg Watu wengine 719 wapatikana na virusi vya COVID-19 huku 800 wakipona

Tue, 29 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Idadi hiyo ilithibitishwa baada ya sampuli 7,608 kupimwa katika saa 24 zilipoitaKati ya visa vipya vilivyorekodiwa Wakenya ni 666 nao raia wa kigeni ni 53Idadi ya maambukizi ya COVID-19 iliongezeka hadi 182,393 baada ya watu wengine 719 kuambukizwa virusi hivyo hatari kutokana na ripoti mpya ya Wizara ya Afya.

Wizara huyo mnamo Jumanne, Juni 29 ilitangaza kuwa idadi hiyo ilithibitishwa baada ya sampuli 7,608 kupimwa katika saa 24 zilipoita.

Takwimu kutoka Wizara hiyo aidha zimefichua kuwa jumla ya sampuli zilizopimwa tangu Mwezi Machi kisa cha kwanza cha coronavirus kilipotua nchini zimefika 1,953,344.

"Kati ya visa vipya vilivyorekodiwa Wakenya ni 666 nao raia wa kigeni ni 53. 435 ni wanaume na wanawake ni 284. Mgonjwa mwenye umri wa chini ni mtoto wa mwaka mmoja naye mkongwe zaidi ana miaka 93," taarifa ya Wizara ya Afya ilisema.

Aidha wagonjwa 1,088 wamelazwa katika hospitali mbali mbali nchini nao 6,465 wanahudumiwa wakiwa manyumbani mwao. Wagonjwa wengie 112 nao wamelazwa wakiwa hali mahututi.

Idadi ya waliopata nafuu nchini imetimia 125,388 baada ya wagonjwa wengine 800 kuripotiwa kupona.

Wagonjwa 695 walikuwa wakipokea matibabu nyumbani nao 695 walikuwa wakihudumiwa katika hospitali mbali mbali.

Wakati uo huo, idadi ya vifo vilivyosababishwa na COVID-19 imefikia 3,574 baada ya wagonjwa 9 kufariki dunia.

Maambukizi yalirekodiwa kama ifuatavyo;

Nairobi 188, Busia 76, Kisii 57, Siaya 53, Kisumu 38, Kilifi 38, Uasin Gishu 29, Kakamega 26, Nakuru 23, Vihiga 22, Mombasa 17, Bungoma 16, Homa Bay 15, Machakos 14, Kericho 13, Turkana 13.

Nandi 11, Kiambu 11,Laikipia 10, Taita Taveta 7, Embu 6, Kajiado 6, Nyamira 5, Kwale 4, Makueni 4, Trans Nzoia 3, Nyeri 2, Kirinyaga 2, Kitui 2, Migori 2, Narok 1, Nyandarua 1, Garissa 1, Isiolo 1, Meru 1 na Bomet 1.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke