Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu wengine 344 wapatikana na virusi vya COVID-19, 11 waaga dunia

722581f83c9b89fc Watu wengine 344 wapatikana na virusi vya COVID-19, 11 waaga dunia

Tue, 15 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Watu wengine 344 wamepatikana na virusi vya corona baada ya sampo 3,654 kufanyiwa vipimo chini ya saa 24 zilizopitaWagonjwa 11 zaidi wamepoteza maisha yao kutokana na makali ya virusi hivyo, kwa jumla idadi ya vifo imefikia 3, 421Kwa sasa jumla ya idadi ya wagonjwa waliopona kutokana na virusi hivyo ni 120, 359 tangu kisa cha kwanza kiliporipotiwa nchini mwezi Machi mwaka wa 2020Wizara ya afya imetangaza kwamba watu wengine 344 wamepatikana na virusi vya corona baada ya sampo 3,654 kufanyiwa vipimo chini ya saa 24 zilizopita.

Kwa jumla idadi ya visa vya maambukizi nchini imefikia 175, 681 huku idadi ya sampo zilizopimwa ikigonga 1, 870, 479.

Kulingana na wizara ya afya, watu wengine 11 wamepoteza maisha yao kutokana na makali ya virusi hivyo, kwa jumla idadi ya vifo imefikia 3, 421.

Wagonjwa wengine 151 wamepona, kati yao 127 walikuwa chini ya utunzi wa nyumbani ilhali 24 walikuwa wakitibiwa hospitalini.

Kwa sasa jumla ya idadi ya wagonjwa waliopona kutokana na virusi hivyo ni 120, 359 tangu kisa cha kwanza kiliporipotiwa nchini mwezi Machi mwaka wa 2020.

Wagonjwa ambao wamelazwa hospitalini kwa sasa ni 961 ilhali 4,770 wamewekwa karatini, wengine 156 wamo katika vyumba vya ICU, 28 wako kwenye ventileta, 108 wako kwenye oksjeni na 20 wanachunguzwa.

Kulingana na kaunti, Nairobi inaendelea kuongoza kwa idadi ya maambukizi ikiwa na 130 ikifuatwa na Kisumu 47, Uasin Gishu 37, Siaya 19, Bungoma 10, Busia na Mombasa 9 kila moja, Nandi, Kakamega, Trans Nzoia na Kilifi visa 8 kila moja, Kisii na Nakuru visa 6 kila moja.

Kaunti za Laikipia, Machakos na Homa Bay visa vitano kila moja huku Kiambu 4, Kajiado na Meru visa vitatu kila moja.

Kwale, Elgeyo Marakwet, Nyandarua, Nyeri na Taita Taveta visa viwili, Baringo, Nyamira na Bomet kisa kimoja.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke