Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu wa Gaza walionaswa kanisani wahofia kupigwa risasi, jamaa asema

Watu Wa Gaza Walionaswa Kanisani Wahofia Kupigwa Risasi, Jamaa Asema Watu wa Gaza walionaswa kanisani wahofia kupigwa risasi, jamaa asema

Mon, 18 Dec 2023 Chanzo: Bbc

Raia walionaswa katika kanisa moja katika Jiji la Gaza wanaishi katika hali ya hofu, jamaa wa mmoja wa walio huko amesema.

Fifi Saba, ambaye dada yake amenaswa ndani ya Kanisa la Holy Family, alisema watu walikuwa na hofu ya kuhama kwa hofu ya kupigwa risasi.

Wanawake wawili waliuawa ndani ya kanisa kwa risasi Jumamosi, Jeshi la Israel limesema halikupata ushahidi wowote kuwa wanajeshi wake walihusika.

Bi Saba, Mkatoliki kutoka Gaza ambaye sasa anaishi Marekani, alikiambia kipindi cha BBC Radio 4 kwamba alikuwa na wasiwasi kuhusu dada yake, shemeji yake na watoto wao wawili wenye umri wa miaka 9 na 12, ambao walikuwa wamenaswa huko.

Alisema alikuwa akipokea habari kuwahusu kupitia mwanafamilia, ambaye aliweza kuzungumza na dada yake mara moja kwa siku.

Hawana simu zao, hawana mtandao, hawana habari." Alisema dada yake mara nyingi aliuliza habari kuhusu kile kinachotokea nje, na aliweza kusikia mabomu angani. "Hofu ambayo wamekuwa wakiishi nayo," alisema.

Chanzo: Bbc