Mon, 24 Jul 2023
Chanzo: Bbc
Jeshi la Sudan linasema watu tisa wamefariki katika ajali ya ndege iliyotokea katika uwanja wa ndege wa Port Sudan.
Ilisema ndege ya kiraia ya Antonov ilipata hitilafu ya kiufundi ilipokuwa ikipaa.
Wanajeshi wanne walikuwa miongoni mwa waliofariki.Msichana mdogo anaripotiwa kunusurika kwenye ajali hiyo.
Zaidi ya watu milioni tatu wameyakimbia makazi yao tangu mapigano kati ya jeshi na wanamgambo wa RSF yalipozuka katikati ya mwezi wa Aprili, huku mzozo huo ukiwa hauonyeshi dalili za suluhu.
Chanzo: Bbc