Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu saba wafariki kwenye ajali Garissa

Watano Wanusurika Kifo Ajali Ya Lori Watu saba wafariki kwenye ajali Garissa

Fri, 12 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Watu saba walifariki katika ajali ya barabarani iliyohusisha basi na tela karibu na kituo cha biashara cha Katumba kwenye barabara ya Garissa-Mwingi.

Kulingana na ripoti ya polisi ,kisa hicho kilijiri wakati dereva wa basi alipogonga trela lililokuwa limekwama barabarani kutokana na kuharibika.

Dereva wa basi hilo lililokuwa likisafirisha abiria 50 kutoka Garissa kuelekea Nairobi, alijaribu kulipita gari lisilojulikana ambalo halikusimama, na kumfanya arudi kwenye njia yake.

Hii, hata hivyo, haikufaulu kwani dereva aliishia kugonga trela iliyokwama. "Kutokana na ajali hiyo, watu 7 wamethibitishwa kufariki huku wengine kadhaa wakikimbizwa katika hospitali mbalimbali," sehemu ya ripoti ya polisi ilidokeza.

Maafisa wa polisi wa trafiki walifika eneo la tukio kurejesha mtiririko wa trafiki kando ya barabara.Uchunguzi zaidi unafanyika.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live