Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu saba wafariki Dunia kwenye Tamasha la Injili

PRAYERSZ KIFOO Watu saba wafariki Dunia kwenye Tamasha la Injili

Mon, 29 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Takriban watu saba walifariki na wengine kadhaa kujeruhiwa vibaya Jumamosi jioni katika mkanyagano wakati wa tamasha la injili katika Uwanja wa michezo wa Kinshasa, vyombo vya habari vya Congo vilisema.

Mkanyagano huo ulifanyika katika uwanja wa Stade des Martyrs, kaskazini mwa mji mkuu, wakati wa tamasha la mwimbaji wa Congo Mike Kalambay.

Kituo cha umma cha RTNC kilitangaza Jumamosi kupitia mtandao wa kijamii wa X kwamba kumekuwa na “vifo saba na watu kadhaa walikimbizwa hospitalini.

Uwanja huo ambao una uwezo wa kuchukua watu 80,000, ulikuwa na watazamaji 30,000 wakati wa tamasha hilo, kwa mujibu wa waandaji.

Mkanyagano kama huo uliotokea mwaka 2022 katika uwanja huo ambapo ulisababisha vifo vya watu kumi na mmoja, wakiwemo watazamaji tisa na maafisa wawili wa polisi, wakati wa tamasha la nyota wa muziki wa Kiafrika, Fally Ipupa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live