Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu 85 wauawa katika shambulio la anga Nigeria

Watu 85 Wauawa Katika Shambulio La Anga Nigeria Watu 85 wauawa katika shambulio la anga Nigeria

Tue, 5 Dec 2023 Chanzo: Bbc

Takriban raia 85 waliuawa katika jimbo la Kaduna, kaskazini-magharibi mwa Nigeria, katika shambulio la anga wakati wa sherehe za kidini za Waislamu zilizofanyika siku ya Jumapili, afisa wa usimamizi wa dharura wa eneo hilo amesema.

Raia hao "waliuawa kimakosa" na ndege isiyo na rubani ya kijeshi wakati ilipokuwa "ikiwalenga magaidi na majambazi", kulingana na Gavana wa jimbo Uba Sani, ambaye hakutoa idadi ya waliouawa.

Wizara ya ulinzi iliitaja operesheni hiyo kama "janga lisilo la lazima".

Makumi wamejeruhiwa wakati wa shambulio hilo.

Afisa wa serikali, Samuel Aruwa, alisema afisa wa jeshi "Maj VU Okoro, amesema kuwa jeshi la Nigeria lilikuwa kwenye harakati zake za kijeshi za kawaida dhidi ya magaidi lakini zimewaathiri wanajamii bila kukusudia".

Katika taarifa yake siku ya Jumanne, Msemaji wa wizara ya ulinzi Meja Jenerali Edward Buba alisema shambulio hilo la anga lilitokana na taarifa za kijasusi kuhusu kuwepo kwa "magaidi" katika eneo hilo.

Gavana Sani ameagiza uchunguzi ufanywe kuhusu "tukio la kusikitisha" lililotokea wakati wanakijiji kutoka Tundun Biri walipokusanyika kwa tamasha la kidini la Jumapili jioni.

"Ofisi ya Kanda ya Kaskazini-Magharibi imepokea taarifa kutoka mamlaka za mitaa kwamba miili 85 hadi sasa imezikwa huku msako ukiwa bado unaendelea," taarifa kutoka kwa Wakala wa Kitaifa wa Usimamizi matukio ya dharura katika mji mkuu wa shirikisho, Abuja, ilisema.

"Inastahili kuzingatiwa kuwa waliojeruhiwa ni watoto, wanawake na wazee."

Mtu mmoja, ambaye alishuhudia kilichotokea, aliambia BBC, kwamba kulikuwa na mashambulizi mawili.

Chanzo: Bbc