Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu 81 ndio waliokuwa eneo la jengo lililoporomoka Afrika Kusini

Aliyenaswa Chini Ya Jengo Lililoporomoka Afrika Kusini Atuma Ujumbe Kwa Familia Watu 81 ndio waliokuwa eneo la jengo lililoporomoka Afrika Kusini

Thu, 9 May 2024 Chanzo: Bbc

Watu 81 ndio waliokuwa katika eneo la jengo lililoporomoka Afrika Kusini Wafanyakazi 81 sasa wamethibitishwa kuwa walikuwa kwenye eneo wakati jengo katika mji wa George wa Afrika Kusini linapoporomoka.

Mamlaka ya eneo hilo ilithibitisha takwimu mpya ikitoa uhakiki wa rekodi za usalama za mwanakandarasi.

Idadi hiyo inatolewa wakati waokoaji wakipambana dhidi ya muda muhimu katika uokoaji wa saa 72 kutafuta manusura.

Shughuli za uokoaji ziliendelea nyakati za usiku kwa kutumia vivunja zege pamoja na lori kuondoa vifusi.

Katika taarifa iliyotolewa Alhamisi asubuhi mamlaka ya eneo hilo ilisema jumla ya watu 37 hadi sasa wamepatikana, na vifo vinane na watu 44 bado hawajulikani waliko.

Chanzo: Bbc