Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu 7 wauawa katika shambulio la kujitoa mhanga Somalia

Watu 7 Wauawa Katika Shambulio La Kujitoa Mhanga Somalia Watu 7 wauawa katika shambulio la kujitoa mhanga Somalia

Thu, 22 Jun 2023 Chanzo: Voa

Takriban watu saba waliuawa Jumatano wakati magari mawili yaliyobeba vilipuzi, yalipolipulika nje ya kambi ya mafunzo ya kijeshi katika mji wa Bardhere, kusini mwa Somalia.

"Wanamgambo hao waliwalenga wanajeshi wa kikanda, kwa mabomu mawili ya kwenye gari. Wanajeshi saba waliuawa na takriban 18 kujeruhiwa,” Osman Nuh Haji, naibu gavana wa eneo la Gedo anayehusika na usalama, aliiambia VOA.

Katika mahojiano na Sauti ya Amerika, mkuu wa wilaya ya Bardhere, Mohamed Wali Yusuf, alisema vikosi vya usalama vya mkoa, vilizuia mabomu ya kujitoa mhanga, ya kwenye gari, kufikia kambi inayotumika kwa ajili ya kuwaajiri watu.

"Tulikuwa tumepata vidokezo vya kiusalama kuhusu uwezekano wa mashambulizi, na hilo lilitusaidia kuzuia mashambulizi na kuzuia magari ya kujitoa muhanga kufikia eneo hilo," alisema Yusuf.

Wanamgambo wenye itikadi kali wa Al-Shabab walidai kuhusika na shambulizi hilo, wakisema "walilenga kambi hiyo kwa sababu maafisa wa Ethiopia na Somalia walikuwa wakikutana huko." Hata hivyo, mamlaka za eneo hilo zimekanusha madai hayo.

Mwezi Machi mwaka huu, shambulio kama hilo la bomu lililotegwa ndani ya gari, lililenga hoteli katika eneo hilo na kusababisha vifo vya wanajeshi kadhaa, na wengine 10 kujeruhiwa.

Chanzo: Voa