Sat, 1 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kwa mujibu wa taarifa ya Mashuhuda, ajali imetokea eneo la Londiani Nchini Kenya baada ya Lori kupoteza uelekeo na kuwafuata waenda kwa Miguu, Wafanyabiashara na Mabasi madogo ya Abiria yaliyoegeshwa kando ya Barabara.
Kamanda wa Polisi wa Londiani, Agnes Kunga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa miili ya waliofariki ilikuwa bado iko chini ya 'Kontena' na kwenye Magari yaliyobanwa na Lori hilo.
Zaidi ya Majeruhi 60 wamekimbizwa katika Vituo mbalimbali vya Afya vya Londiani, Kericho na Nakuru. Zoezi la uokoaji limekumbwa na ugumu kutokana na Mvua kubwa zinazonyesha.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live