Zaidi ya watu 30 hawajulikani walipo Kaskazini Mashariki mwa jimbo la Borno nchini Nigeria, baada ya kushambuliwa na vikosi vya watu wenye silaha week end iliyopita.
Mashuhuda wanasema kuwa waathirwa wa tukio hilo wanatokea mji wa Rann , ambapo walifyatuliwa risasi na watu wenye silaha ambao walikua kwenye pikipiki., wakati walipokua porini kutafuta kuni.
Kuna hofu kwamba makumi ya watu wametetwa ama wameuawa
Haijulikani ni nani aliyefanya shambulizi hilo, lakini vikosi vya Boko Haram na vingine vinavyohusiana na dola la kiislamu IS vimekua vikisababisha matukio ya aina hiyo kwenye ukanda huo.
Mamlaka za kijeshi za Nigeria hazijatoa tamko lolote kuhusiana na tukio hilo.