Mon, 29 Apr 2024
Chanzo: Bbc
Watu 20 wamethibitishwa kufariki baada ya mafuriko makubwa kusomba nyumba kadhaa katika Kijiji cha Kamuchiri Mai Mahiu, Kaunti ya Nakuru nchini Kenya kufuatia mvua kubwa iliyonyesha.
Maji ya mafuriko yalitoka kwenye mto ulio karibu ambao ulivunja kingo zake Jumapili usiku, kulingana na Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya.
Kamanda wa polisi wa Naivasha Stephen Kirui amethibitisha kisa hicho akibainisha kuwa wengine kadhaa wamekimbizwa katika hospitali ya Naivasha kwa matibabu.
Chanzo: Bbc