Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu 111 wamekutwa na COVID-19, wengine14 wafariki dunia

COVID Watu 111 wamekutwa na COVID-19, wengine14 wafariki dunia

Tue, 25 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wagonjwa wengine 14 wamefariki dunia kutokana na virusi vya covid-19, jumla ya vifo vilivyoripotiwa nchini kwa sasa ni 3,073

- Watu 111 zaidi wamepatikana na virusi hivyo baada ya sampo 1,948 kufanyiwa vipimo

- Kwa sasa Wagonjwa 121 wamelazwa ICU, kati yao 25 wamewekwa kwenye ventileta, 68 kwenye oksijeni na 28 wako chini ya uangalizi wa madaktari

Wizara ya afya imetangaza kwamba watu 111 zaidi wamepatikana na virusi vya COVID-19 baada ya sampo 1, 948 kufanyiwa vipimo chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya visa hivyo, 108 ni Wakenya ilhali 3 ni raia wa nchi za kigeni, kijinsia, 62 ni wanaume na 46 ni wanawake. Mgonjwa mdogo anaumri wa miaka 2 ilhali mkubwa ana miaka 89.

Kulingana na takwimu za wizara hiyo, jumla ya idadi ya maambukizi imefikia 168,543 huku idadi ya sampo zilizopimwa ikigonga 1,783,374.

Wagonjwa 142 wamepona kutokana na virusi hivyo, 137 walikuwa wamejitenga manyumbani wakipokea matibabu na watano walikuwa wamelazwa katika hospitali mbali mbali.

Kufikia sasa jumla ya idadi ya wagonjwa waliopona nchini imefikia 114, 697.

Aidha, wagonjwa wengine 14 wamepoteza maisha yao kutokana na virusi hivyo chini ya muda wa saa 24 zilizopotia na kupelekea idadi ya vifo kufikia 3,073.

Wagonjwa 1, 086 wamelazwa katika hospitali mbali mbali nchini ilhali 4,770 wako chini ya utunzi wa nyumbani.

Kwa sasa Wagonjwa 121 wamelazwa ICU, kati yao 25 wamewekwa kwenye ventileta, 68 kwenye oksijeni na 28 wanachunguzwa..

Kufikia Jumamosi, Mei 22, watu 954,515 walikuwa wamepokea chanjo ya kudhibiti makali ya virusihivyo, kati yao 289,900 wana kati ya umri wa miaka 58 na kuendelea, 164,053 ni wakiwa wahudumu wa afya, 150,303 ni walimu 80,718 walinzi ilhali 269,541 ni raia wa kawaida.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke