Idadi ya waliofariki katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi ya leo Novemba 6, 2023, katika eneo la Ngata, barabara kuu ya Nakuru- Eldoret imeongezeka na kufikia vifo 11 baada ya watu wengine watano kufariki wakati wakipatiwa matibabu. Miongoni mwa waliopoteza maisha yupo mtoto wa miezi sita pamoja na mama yake mzazi.
Idadi ya waliofariki katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi ya leo Novemba 6, 2023, katika eneo la Ngata, barabara kuu ya Nakuru- Eldoret imeongezeka na kufikia vifo 11 baada ya watu wengine watano kufariki wakati wakipatiwa matibabu. Miongoni mwa waliopoteza maisha yupo mtoto wa miezi sita pamoja na mama yake mzazi. Kamanda wa Polisi wa Kaunti ya Nakuru, Samuel Ndanyi, amesema ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa lori alipopoteza udhibiti wa gari lake na kuacha barabara na kuingia upande wa pili na kugongana uso kwa uso na daladala.