Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu 100 wauwa katika mapigano Darfur

Mapigano Watu 100 wauwa katika mapigano Darfur

Wed, 8 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Zaidi ya watu 100 wameuawa kufuatia mapigano ya kikabila katika jimbo la Dafur Magharibi nchini Sudan.

Mapigano kati ya Waarabu na wapiganaji wa Kiafrika kutoka jamii ya Masalit inayoungwa mkono na waasi wa zamano yamekuwa yakiendelea kwa siku kadhaa sasa.

Mapigano katika eneo la Kreinik yamesababisha maelfu ya watu kutoroka makwao, wengine wakivuka mpaka na kuingia nchi jirani ya Chad, tUmoja wa Mataifa unasema.

Mmoja wa manusura wa ghasia hizo anasema wanaume waliyojihami walishambulia vijiji vyao magharibi mwa Kreinik, na kuanza kupiga risasi kabla ya kuchoma moto nyumba zao.

Pia waliweka vizuizi katika barabara kuu kuwazuia watu kutoroka.

Waliyojeruhiwa hawana njia ya kupata matibabu ya dharura.

Mapigano mapya ya kikabila yalianza Jumapili kati ya jamii hizo mbili, karibu watu 55 wameuawa.

Miili zaidi ilipatikana msituni na kuongeza idadi ya vifo hadi zaidi ya 100. Makumi ya wengine hawajulikani waliko.

Mwezi uliopita, watu 43 waliuawa katika sehemu tofauti ya Darfur Magharibi.

Mapigano ya kikabila pia yameripotiwa kusini mwa eneo hilo lenye machafuko.

Serikali imetuma kikosi cha pamoja cha vitengo vya kijeshi, jeshi na polisi huko Darfur Magharibi na Kusini ili kujaribu kuzuia ghasia.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live