Wed, 4 Sep 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu 10 wanahofiwa kufariki kufuatia ajali mbaya ya barabarani iliyotokea Jumanne katika eneo la Kipsitet, Koguta, kwenye barabara kuu ya Londiani-Muhoroni.
Ajali hiyo ilitokea wakati lori lililokuwa limebeba unga lilipogongana na matatu ya abiria 14 kando ya barabara kuu.
Ripoti za polisi zinaonyesha dereva wa trela alishindwa kulidhibiti, na kuyumba nje ya njia yake na kugongana na matatu iliyokuwa ikielekea Kisumu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live