Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watoto 3 wazama kwenye machimbo ya mawe wakiogelea huko Turkana

53afb7df2942a0ee Watoto 3 wazama kwenye machimbo ya mawe wakiogelea huko Turkana

Mon, 17 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Watatu hao wenye umri wa miaka 11,8 na 6 walikuwa wanachunga mifugo yao wakati waliamua kuogelea ndani ya maji hayo machafu

- Machimbo hayo yanadaiwa kuchimbwa 2011 na Wakimbizi wa Ndani kwa Ndani(IDPS) ambao walikuwa wamekita kambi eneo hilo

- Maiti ya watoto hao ilipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Lodwar ikisubiri kufanyiwa upasuaji

Familia moja Turkana inaomboleza kifo cha watoto watatu ambao walizama ndani ya machimbo ya wazi katika kijiji cha Kampi Mpya.

Watatu hao wenye umri wa miaka 11,8 na 6 walikuwa wanachunga mifugo yao wakati waliamua kuogelea ndani ya maji hayo machafu.

Walioshuhudia kisa hicho cha Jumapili, mei 16, walisema walikuwa wamewaonya watoto hao dhidi ya kuogelea ndani ya machimbo hayo.

Machimbo hayo yanadaiwa kuchimbwa 2011 na Wakimbizi wa Ndani kwa Ndani(IDPS) ambao walikuwa wamekita kambi eneo hilo.

Wakazi wa eneo hilo wameomba serikali kuziba machimbo hayo ili kuzuia ajali kama hiyo siku za usoni.

Maiti ya watoto hao ilipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Lodwar ikisubiri kufanyiwa upasuaji.

Katika taarifa tofauti, marafiki na jamaa Jumamosi, Mei 8, walikusanyika katika kijiji cha Karatina, Kaunti ya Nyeri, kwa mazishi ya watoto watatu ambao waliangamia kwenye mkasa wa moto katika nyumba yao Nakuru.

Leah Njoki, Teresa Wanjiru na Mildred Akal ni binti zake afisa wa polisi wa Nakuru Mary Migwi ambaye hufanyia kazi yake katika kituo cha polisi cha Miti Mingi huko Gilgil lakini makazi yake ni mjini wa Nakuru.

Afisa huyo alikuwa zamu wakati wa ajali hiyo nyumbani kwake, na alikuwa amehamia hapo siku tatu kabla ya tukio hilo.

Watatu hao, wenye umri kati ya miaka 11 na miwili, walizikwa karibu na kila mmoja katika hafla iliyofanywa kwa kufuata sheria kali za Wizara ya Afya dhidi ya COVID-19.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke