Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watawala wa kijeshi wa Niger wakutana na wajumbe wa Nigeria

Watawala Wa Kijeshi Wa Niger Wakutana Na Wajumbe Wa Nigeria Watawala wa kijeshi wa Niger wakutana na wajumbe wa Nigeria

Thu, 10 Aug 2023 Chanzo: Voa

Mazungumzo hayo yalifanyika huku Niger ikiishutumu Ufaransa kwa kukiuka anga yake kushambulia kambi ya kijeshi

Watawala wa kijeshi wa Niger walikutana na wajumbe wawili wa Nigeria siku ya Jumatano na kutoa matumaini kwa mazungumzo kabla ya mkutano na viongozi wa kikanda ambao unaweza kusababisha hatua za kijeshi ili kurejesha demokrasia.

Mazungumzo hayo yalifanyika huku Niger ikiishutumu Ufaransa kwa kukiuka anga yake kushambulia kambi ya kijeshi na kuwaachia huru magaidi ili kuidhoofisha nchi hiyo. Paris ilikanusha madai hayo.

Afisa wa jeshi Amadou Abdramane akizungumza kwa niaba ya viongozi wa mapinduzi alitoa madai hayo katika taarifa ya video bila kutoa ushahidi na hivyo kuzua mvutano kabla ya mkutano wa Alhamisi na wakuu wa nchi za Afrika Magharibi ambao wanatarajiwa kujadili hatua ikiwa ni pamoja na hatua za kijeshi dhidi ya utawala wa kijeshi.

Chanzo: Voa
Related Articles: