Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watahaniwa wa KCSE wakesha Uhuru Park baada ya kunaswa na kafyu

5f7decabb521e29c Watahaniwa wa KCSE wakesha Uhuru Park baada ya kunaswa na kafyu

Tue, 20 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wanafunzi hao ambao walikuwa wamekamilisha Mtihani wa Kidato cha Nne (KCSE) walishindwa kufika makwao kwa sababu ya kafyu

- Serikali iliweka sheria ya kafyu kuanzia saa mbili usiku hadi saa kumi asubuhi katika kaunti za Nairobi, Nakuru, Kiambu, Kajiado na Machakos

- Maafisa wa polisi wamekuwa wakifunga barabara kuu jijini kutekeleza sheria ya kafyu

Watahiniwa wa Kidato cha Nne kutoka shule mbalimbali walikwama katika Bustani la Uhuru, jijini Nairobi mnamo Jumatatu, Aprili 19, usiku kwa sababu ya sheria za kafyu.

Serikali iliweka sheria ya kafyu kuanzia saa mbili usiku hadi saa kumi asubuhi katika kaunti za Nairobi, Nakuru, Kiambu, Kajiado na Machakos kudhibiti kuenea kwa COVID-19.

Wanafunzi hao ambao walikuwa wamekamilisha Mtihani wa Kidato cha Nne (KCSE) walishindwa kufika makwao kwa sababu ya sheria hiyo.

Msongamano mkubwa ulishuhudiwa katikati mwa jiji la Nairobi huku wakazi wakipigana na kafyu.

Serikali imeshikilia kuwa imejitolea kuhakikisha sheria hiyo inafuatwa baada ya wananchi kulegea kufuata sheria za kudhibiti COVID-19.

Baadhi ya walimu na wanafunzi ambao walishikamana waliomba serikali kufungua taifa ama kuongeza saa za kafyu.

Mathew Rotich, ambaye ni mwalimu katika Shule ya Wavulana ya Anestar, kaunti ya Nakuru alisema aliandamana na wanafunzi wake kwa sababu walifanya karatasi ya mwisho wakiwa wamechelewa.

“Wanafunzi wetu walimaliza mtihani wakiwa wamechelewa, wakati tunafika Nairobi, tayari tulikuwa tumechelewa na hakuna kitu tungefanya,” alisema.

Mwalimu huyo alisema ingelikuwa vyema kwa serikali kuwapa walimu na wanafunzi muda wa kutosha kufika nyumbani kwao bila kutatizwa.

"Hali ya sasa ni ngumu kwa walimu na wanafunzi wanaosafiri nyumbani kwa sababu wanakimbizana na muda.Na ili kuweza kuwai mapema kuna mambo kadhaa ya kuzingatia kama msongamano, baadhi ya wazazi wanatakiwa kuwachukuwa wanao na changamoto kadhaa barabarani," alisema Rotich.

Maafisa wa polisi wamekuwa wakifunga barabara kuu jijini kutekeleza sheria ya kafyu.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke