Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Washirika wa Nato wapinga wazo la Macron la kupeleka wanajeshi Ukraine

Washirika Wa Nato Wapinga Wazo La Macron La Kupeleka Wanajeshi Ukraine Washirika wa Nato wapinga wazo la Macron la kupeleka wanajeshi Ukraine

Wed, 28 Feb 2024 Chanzo: Bbc

Nchi kadhaa za Nato, zikiwemo Marekani, Ujerumani na Uingereza, zimefutilia mbali pendekezo la kupeleka wanajeshi wa ardhini nchini Ukraine, baada ya Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kusema "hakuna lisilowezekana".

Bw Macron alisema "hakuna makubaliano" yaliyofikiwa juu ya kutuma wanajeshi wa mataifa ya Magharibi nchini Ukraine.

Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov ameonya kuhusu mzozo wa moja kwa moja ikiwa wanajeshi wa Nato watatumwa huko.

Vikosi vya Urusi hivi karibuni vimepata mafanikio nchini Ukraine na Kyiv imeomba kwa dharura silaha zaidi.

Bw Macron aliambia mkutano wa wanahabari Jumatatu jioni: "Hatupaswi kuwatenga kwamba kunaweza kuwa na hitaji la usalama ambalo linahalalisha baadhi ya vipengele vya kupelekwa.

"Lakini nimekuambia kwa uwazi kabisa kile ambacho Ufaransa inashikilia kama msimamo wake, ambao ni utata wa kimkakati ambao ninasimama nao."

Kiongozi huyo wa Ufaransa alikuwa akizungumza mjini Paris, ambayo ni mwenyeji wa mkutano wa mgogoro wa kuunga mkono Ukraine, unaohudhuriwa na wakuu wa mataifa ya Ulaya, pamoja na Marekani na Canada.

Uvamizi kamili wa Ukraine ulioanzishwa na Rais wa Urusi Vladimir Putin sasa ni mwaka wa tatu, na hakuna dalili kwamba vita hiyo kubwa zaidi barani Ulaya tangu Vita vya Pili vya Dunia vinaweza kumalizika hivi karibuni.

Kauli ya Bw Macron ilivutia hisia kutoka kwa nchi nyingine za Ulaya na wanachama wa Nato.

Rais wa Marekani Joe Biden anaamini "njia ya ushindi" ni kutoa msaada wa kijeshi "ili wanajeshi wa Ukraine wawe na silaha na risasi wanazohitaji kujilinda", taarifa ya Ikulu ya White House ilisema.

"Rais Biden amekuwa wazi kwamba Marekani haitatuma wanajeshi kupigana nchini Ukraine," iliongeza.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amesema hakujakuwa na mabadiliko yoyote katika msimamo uliokubaliwa kuwa hakuna nchi yoyote ya Ulaya au nchi mwanachama wa Nato itakayotuma wanajeshi wake nchini Ukraine.

Msemaji wa Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak alisema kuwa nchi hiyo haina mpango wa kupeleka wanajeshi wengi nchini Ukraine, zaidi ya idadi ndogo ya wafanyakazi ambao tayari wanatoa mafunzo kwa vikosi vya Ukraine.

Chanzo: Bbc