Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wapenzi wafungwa miezi 30 baada kwa kufanya ngono hadharani

Be6159fbb2e946e6 Wapenzi wafungwa miezi 30 baada kwa kufanya ngono hadharani

Thu, 11 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wanandoa nchini Uganda wamefungwa jela kwa miezi 30 baada ya kunaswa kwenye video wakifanya mapenzi katikati ya barabara yenye shughuli nyingi.

Paskari Hafashimana na mpenzi wake Colodine Mukamulenzi Muhawenimana walifumaniwa wakifanya mapenzi kando ya barabaraVideo ya wapenzi hao wawili ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii na kuwavizia maafisa wa usalama kuwakamata.

Hafashimana na Muhawenimana walifikishwa mbele ya hakimu Fred Gidudu ambapo walikubali kuwa na hatia katika mashtaka yote dhidi yao.

Paskari Hafashimana,29, na mpenzi wake Colodine Mukamulenzi Muhawenimana, 24, walinaswa kwenye vieo wakishiriki ngono mchana peupe karibu na baiskeli iliyokuwa imeegeshwa kwenye barabara ya Kisoro-Bunagana.

Tuvuti ya Uganda, Nile Post siku ya Jumatano, Novemba 10, iliripoti kuwa video ya wapenzi hao wawili ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii na kuwavizia maafisa wa usalama.

Kisha wawili hao walikamatwa na polisi kwa usumbufu hadharani lakini Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Uganda alifungua kesi ya kufanya kitendo kisichofaa dhidi yao.

Wakiri makosaHafashimana na Muhawenimana walifikishwa mbele ya hakimu Fred Gidudu ambapo walikubali kuwa na hatia katika mashtaka yote dhidi yao.

Hata hivyo, waliomba kutopewa adhabu kali huku Gidudu akiwafunga jela kwa miezi 30.

Wafanya ngono katika bustani ya UhuruMnamo 2019, mahakama nchini Kenya mwanamume mmoja alipigwa faini ya KSh 1,500 kwa kosa la kushiriki ngono hadharani katika bustani ya Uhuru Park jijini Nairobi.

Kanara Maina na mpenzi wake Joyce Wanjiku walipatikana na maafisa wa Kaunti ya Nairobi wakifanya kitendo hicho hadaharani.

Katika hukumu hiyo ilitolewa na hakimu Joseline Onga'yo mnamo Jumatatu, Mai 29, wawili hao walipatikana na makosa ya kukiuka sheria za kaunti ya Nairobi ya kushiriki tendo la ndoa hadharani.

Maina alikubali makosa yake na kuiomba korti radhi na kuapa kutorudia tena kosa hilo.

Wawili hao walifumaniwa wakishiriki ngono na baadaye kuachiliwa huru kwa dhamana ya KSh 500.

Wanjiku alishindwa kufika mahakamani kusikiza kesi hiyo dhidi yake.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke