Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waokoaji wawaondoa wachimba migodi 15 wa Zimbabwe

Waokoaji Wawaondoa Wachimba Migodi 15 Wa Zimbabwe Waokoaji wawaondoa wachimba migodi 15 wa Zimbabwe

Mon, 8 Jan 2024 Chanzo: Bbc

Wachimba migodi wote kumi na watano waliokuwa wamenaswa katika mgodi wa dhahabu wa Zimbabwe kwa siku nne wameokolewa.

Waziri wa Madini Soda Zhemu alisema wafanyakazi walikuwa na afya njema na fahamu.

Mgodi wa dhahabu wa Redwing unaomilikiwa na Metallon Corporation uliporomoka siku ya Alhamisi.

Maafisa walisema tetemeko la ardhi huenda lilisababisha ajali hiyo.

Familia za wafanyakazi waliokwama wamekuwa wakipiga kambi katika eneo la mgodi katika kijiji cha uchimbaji madini cha Penhalongato - kilomita 270 (maili 167) mashariki mwa mji mkuu Harare - wakisubiri uokoaji.

Eneo hilo ni nyumbani kwa wafanyikazi wengi wasio na hati ambao hutafuta riziki huku kukiwa na hali ngumu ya kiuchumi.

Chanzo: Bbc